Posts

SHENG' NA USANIFISHAJI WAKE

Image
  Nilishangazwa ajabu Profesa Kimani Njogu, Profesa Mukoma wa Ngugi, Bi. Jane Obuchi na Kilolo Munyao waliposhabikia na kuwa makini kusikilizi mwandishi wa Sheng’ Felix Omondi akiwasilisha tafsiri yake ya kifungu cha bibilia tulichopewa kutafsiri wakati wa kongamano la Ituika agosti 12 mjini Naivasha. Pamoja na kwamba washiriki wengi walikuwa ama wandishi wa Kiswahili au wapenzi wake ukumbi ulichangamka wakati Felix Omondi alikuwa anatoa wasilisho lake. Binafsi sikutarajia kwani mara kwa mara jamii ya wapenzi wa Kiswahili imetaja sheng’ kuwa maradhi katika makuzi ya Kiswahili. Baada ya hapo tuliingia kwenye mjadala mkali ulioendelea hadi saa kumi asubuhi siku   iliyofuatia. Majadiliano hayo yalihusisha Paul Nganga, Dr. Maina Mutonya, Dr. Kuria na Dr. Dosline. Miongoni mwa mengi yaliyojadiliwa ni wasilisho la Felix Omondi. Wanne hao walinifunza mimi jogoo wa shamba mengi nisiyoyajua kuhusu Sheng'. Kwanza ni kuwa Sheng' huwa na 'lahaja' zake kwa kutegemea sehemu au ene...

MATHIAS MOMANYI APENDEKEZA USAWA KATIKA TUZO ZA KISWAHILI

Image
  M.Momanyi :  “LINAYAVUNJA MATAIFA MENGINE MOYO… SAWAZISHA. UTAIFA NI UPI?” Mwanahabari Mathias Momanyi alitia doa kwenye uamuzi wa majaji wa Tuzo za Kiswahili zinazothaminiwa na chuo kikuu cha Cornell, Shirika la Mabati Rolling na wakfu wa Ngugi wa Thiong’o. Kwenye mkutano wa mtandaoni ulioshirikisha karibia watu mia moja kutoka mataifa tofauti tofauti, wakenya walibaki vinywa wazi   baada ya Profesa Abdilatiff Abdalla kufichua kuwa washiriki wote waliotinga orodha ya saba bora walitoka katika taifa la Tanzania. Isitoshe akiwapa moyo washiriki waliotuma miswada yao ila hawakufaulu kuingia kwenye orodha hiyo, Prof. Alifichua kuwa asilimia 70 ya miswada yote ilitoka katika taifa la Tanzania. Ufichuzi huo haukuwafurahisha baadhi ya Wakenya waliokuwa mkutanoni, mwanahabari Mathias Momanyi akitoa hisia na mapendekezo yake kuhusiana na suala lenyewe.   “HAPA KAZI IPO... RIZIKI YAZIBWA AU YAWANIWA ” Momanyi alitaja mwelekeo huo kuwa wa kuvunja moyo wandishi wa ...